Psalms 8:1-4

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi.

1 aEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako
juu ya mbingu.
2 bMidomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao
umeamuru sifa,
kwa sababu ya watesi wako,
kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 cNikiziangalia mbingu zako,
kazi ya vidole vyako,
mwezi na nyota,
ulizoziratibisha,
4 dmwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,
binadamu ni nani hata unamjali?
Copyright information for SwhNEN